Header Ads

Header ADS

Menina Abdulkarim hatimaye ameitikia wito wa BASATA.

    Menina Abdulkarim ambae ni muigizaji wa filamu nchini laki ni pia msanii wa bongo fleva  na MC nchini ameweza kukubali uwito na kuwasili katika Ofisi za Baraza la sanaa la Taifa(BASATA)zinazopatika sharifu shamba,Ilala Jijini Dar es salaam kwa ajili ya maojiano kuhusu picha na video zilizosambaa katika mitandao ya kijamii za utupu.
  Katika maojiano hayo BASATA wameweza kusikiliza maelezo ya Menina pia sababu au chanzo kilichopelekea kusambaa kwa video hizo katika mitandao ya kijamii.














Ambapo BASATA imesema Kwa kuwa suala la kusambaa video na picha za utupu za Msanii Menina katika mitandao ya kijamii lipo mikononi mwa mamlaka nyingine, imeamua kuyafanyia kazi maelezo yake.
  Ambapo Godfrey L.Mngereza Katibu Mtendaji-BASATA.ametoa taarifa hiyo.
     Lakini pia,BASATA kupitia utaratibu wake wa kutoa Elimu kwa wasanii na Umma mara kadhaa wamekuwa wakiwaonya au kuwaelekeza wasanii kuhusu utendaji wa kazi zao na kuwataka kuzingatia maadili ya jamii katika kazi zao,hata hivo kufuata taratibu za kujisajiri lakini baadhi ya wasanii hujikuta wanafunza maadili ya nchi kutokana na kwenda kinyume au kutofuata maagizo wanayopewa katika Elimu inayotolewa kwao.
    
    
   

No comments

Powered by Blogger.