Header Ads

Header ADS

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma yatoa kanusho la taarifa ya wanafunzi 350 kuacha shule.

    Katika taarifa zilizotolewa na Gazeti la Habari Leo la tarehe 28 Oktoba 2019 na Kituo cha Televisheni cha ITV ikisomeka kuwa “Wanafunzi 350 waacha shule kwa utoro, mimba,”Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma inapenda kukanusha habari hiyo ya upotoshaji na kueleza kuwa  habari hii haina ukweli wowote kama ilivyoripotiwa.
     Tunapenda kuuarifu umma kuwa baada ya kuwepo kwa taarifa hiyo Ofisi ya Mkurugenzi imefanya ufuatiliaji wa kina katika Shule ya Sekondari Marumba ambayo imetajwa katika habari hiyo iliyosema kuwa wanafunzi 350 wa shule hiyo wameshindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya utoro na mimba kwa kipindi cha miaka minne mfululizo  kuanzia mwaka 2016 hadi 2019.
     Ni vyema umma ukafahamu kuwa katika kipindi cha miaka minne yaani 2016 hadi 2019, shule hii ilipangiwa idadi ya wanafunzi 603 ikiwa wavulana 320 na wasichana 283, waliosajiliwa kwa kipindi hicho ni wanafunzi 515 ikiwa pungufu ya wanafunzi 88 kati ya waliopangwa. 










    Aidha,Takwimu zinaonesha kuwa idadi ya wanafunzi waliopo katika shule ya Sekondari Marumba hadi kufikia tarehe 28/10/2019 ni 345 ikiwa wavulana 208 na wasichana 137 kukiwa na upungufu wa wanafunzi 170.  
   Gasper Balyomi ambae ni Mkurugenzi Mtendaji Halmasahuri ya Tunduru akitoa ufafanuzi huo amesema hii ni wazi kuwa idadi ya wanafunzi 350 wa sekondari ya Marumba walioripotiwa hawajulikani walipo hazina ukweli wowote kufuatia takwimu zilizotolewa na kubaini kuwa:- 
1.Kwa kipindi cha miaka minne mfululizo jumla ya wanafunzi 20 walihama kwenda katika shule nyingine. 
2.Wanafunzi 15 waliacha masomo baada ya kupata ujauzito
3.Wanafunzi 63 waliacha masomo kutokana na sababu mbalimbali
4.Wanafunzi 72 waliopewa nafasi ya kurudia masomo baada ya kufeli  kidato cha pili  baadhi yao wazazi waliamua kuwapeleka katika vyuo vya Ufundi stadi kama  (VETA) na shule binafsi.
  Ambapo  jumla ya wanafunzi 170 kwa kipindi cha miaka minne ndio hawapo shuleni tofauti na taarifa ilivyoonesha jumla ya wanafunzi 350 wa shule hiyo wameacha masomo.
Lakini pia kuhusu suala la utoro wa reja reja Halmshauri inaendelea kushirikiana na wazazi pamoja walezi wa wanafunzi katika kuahikisha utoro mashuleni unadhibitiwa. 
   

No comments

Powered by Blogger.