Header Ads

Header ADS

Rais Magufuli Asamehe Wafungwa 5,533

     Leo ni Siku ya kusherekea miaka 58 ya Uhuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, ametangaza kuwaachia wafungwa 5533 ambao walikuwa wamefungwa katika Magereza mbalimbali nchini.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho wa miaka 58 ya Uhuru wa Tanzania Bara, ambapo kuna idadi kubwa ya wafungwa ambao wapo Magerezani kwa makosa ya kawaida sana.“Nilitembelea Magereza nikashuhudia kuna mlundikano wa wafungwa, mpaka leo kuna Wafungwa 17,547 na Mahabusu 18,256, hii ni idadi kubwa, kwa hao wafungwa kuna baadhi wamefungwa makosa madogo, sijui kaiba kuku, kujibizana na mpenzi wake.“Leo natangaza kuwasamehe wafungwa 5,533, ni mara ya kwanza kwa msamaha mkubwa kama huu kutokea, najua watu watashangaa lakini nimetumia siku hii ya Uhuru kusamehe, sifurahi kuongoza nchi yenye watu wengi Magerezani.
“Msamaha huu utawahusisha wafungwa waliofungwa kati ya kipindi cha siku moja hadi mwaka mmoja, na wale Wafungwa waliofungwa Miaka mingi kama 30, 20, 10 au mitano na wamebakiza muda mfupi kumaliza. Aliyewasamehe ni Mungu.” Rais Magufuli.

No comments

Powered by Blogger.