Header Ads

Header ADS

Bajaji zinazofanya kazi kinyemela zaongezeka Njombe.

   Umoja wa wamiliki wa pikipiki za magurudumu matatu maarufu kama bajaji mkoani Njombe, kulalamikia ongezeko la bajaji zaidi ya ishirini ambazo zinadaiwa kufanya kazi ya usafirishaji wa abiria kinyume na sheria, mamlaka ya udhibiti wa usafiri ardhini Latra pamoja na mamlaka ya mapato TRA wamesema wamejipanga kufanya oparesheni ya ghafla kuvibaini vyombo hivyo na kuchukua hatua za kisheria.

   Hata hivyo,  Sakata  la mgogoro wa kimaslahi baina ya madereva bajaji na daladala lilifurukuta mwishoni mwa mwaka jana na likamlazimu mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka kukutana na pande hizo mbili na kutoa ruhusa ya ongezeko la bajaji 49 kutoka 51 na kufikia 100 ili kukidhi mahitaji ya watu mjini humo jambo ambalo lilipokewa vyema na wananchi wa mkoa huo.

No comments

Powered by Blogger.