Header Ads

Header ADS

Spika Ndugai Aomboleza Kifo cha Mbuge

             Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, amesema kuwa ofisi yake inaendelea kuratibu mipango ya mazishi ya Mbunge wa Newala Vijijini, Rashid Akbar, aliyeaga Dunia leo Januari 15, 2020, Mingoyo mkoani Lindi.

  Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Spika Ndugai amepokea taarifa za msiba huo kwa masikitiko makubwa na kutoa pole kwa wanafamilia wote.

"Natoa pole kwa wafiwa wote wakiwemo familia ya marehemu, Waheshimiwa Wabunge, ndugu, jamaa na marafiki. Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu" amesema Spika Ndugai.
  

No comments

Powered by Blogger.