Header Ads

Header ADS

Benard Membe Atimuliwa CCM....Makamba Asamehewa, Kinana Apewa Karipio kali

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa CCM ikiongozwa na Mwenyekiti na Rais wa Tanzania Dkt Magufuli katika kikao cha kawaida cha Kamati hiyo kilichoketi leo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba, DSM imeazimia kumfukuza uanachama Bernard Membe.

Katibu Mkuu Mstaafu wa chama hicho Yusuf Makamba, amesamehewa kutokana na kuomba kusamehewa makosa aliyokuwa akidaiwa kuyatenda  ya kwenda kinyume na maadili ya chama hicho. 
  Aidha, Katibu Mkuu Mstaafu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana,amepewa adhabu ya kalipio kali  kwa mujibu wa kanuni za uongozi na maadili ya chama hicho  na atakuwa kwenye uangalizi  kwa kipindi cha miezi 18.

No comments

Powered by Blogger.