Header Ads

Header ADS

Ndege za kivita za Israel zatumia ndege ya abiria kama ngao Syria

      Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema ndege za kijeshi za Israel zimetumia ndege ya abiria kama ngao ya kujikinga katika uvamizi wake mpya dhidi ya Syria.
     Msemaji wa wizara hiyo, Meja Jenerali Igor Konashenkov alisema jana Ijumaa kuwa, ndege ya abiria ya Airbus-320 iliyokuwa na abiria 172 nusra ipigwe na makombora ya mfumo wa Kujikinga ya Syria kielekea Damascus kutoka Tehran wakati ndege za Kijeshi za Israel zilipofanya mashambulizi.
Hata hivyo mfumo wa ngao ya makombora ya Syria mjini Damascus ulifanikiwa kutungua makombora hayo ya  Israel.

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi ameeleza bayana kuwa, baada ya kukoswakoswa na makombora , ndege hiyo ya abiria ililazimika kutua kwa dharura katika uwanja wa kijeshi wa Hmeymim katika mkoa wa pwani wa Latakia, magharibi mwa Syria.

Meja Jenerali Konashenkov amekosoa mienendo hiyo ya Israel ya kufanya mashambulizi yake ya makombora bila kujali ndege za abiria zinazoruka katika anga ya Syria

No comments

Powered by Blogger.