Header Ads

Header ADS

Urusi na Ukraini zarushiana makombora

  Ukraine imesema mwanajeshi wake mmoja ameuawa na wengine kadhaa wamepata majeraha, katika makabaliano na vikosi vya Urusi ambavyo Ukraine imesema viliingia kwenye ardhi yake.
   Tangazo la wizara ya ulinzi limesema kuwa mapigano hayo yalitokea katika mikoa minne ya mashariki mwa Ukraine ambayo ina wakaazi wachache.
Wizara hiyo imesema imeweza kujibu mapigo ya iliyemtaja kuwa adui yake, na kuweza kudhibiti hali ya mambo katika mkoa wa Luhansk.

Aidha, kulingana na tangazo hilo, mwanajeshi mmoja wa upande wa wanamgambo wanaoungwa mkono na Urusi ameuawa pia.

Kila upande unaushutumu mwingine kuvunja makubaliano yaliyosainiwa, yakihimiza kuondolewa kwa silaha nzito nzito.

Wiki iliyopita, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy alifanya mazungumzo na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin kwa njia ya simu, ambapo walikumbushana makubaliano mapya ya amani yaliyotiwa saini mjini Paris miezi miwili iliyopita.

No comments

Powered by Blogger.