Header Ads

Header ADS

Zitto Kabwe Achukua Fomu Kutetea Tena Nafasi Yake Ndani ya Chama cha ACT Wazalendo

     Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe leo Februari 18, jijini Dar es Salaam amechukua fomu ya kuomba kugombea tena nafasi hiyo kwa muhula mwingine. 
   Akizungumza baada ya kuchukua fomu, Zitto amesema ameamua kutetea nafasi hiyo kwa awamu ya pili baada ya kushauriana na watu mbalimbali ikiwemo familia yake.
 “Nimechukua tena fomu ya kugombea uongozi wa chama katika uchaguzi utakaofanyika katika mkutano wa chama utakaoanza Machi 14 hadi 16, 2020.”

“Mimi nimeshatumikia muhula mmoja na kwa mujibu wa Katiba yetu mihula ni miwili, kwa hiyo naomba muhula huu wa pili na wa mwisho kwa mujibu wa katiba ya ACT-Wazalendo,” amesema Zitto.

No comments

Powered by Blogger.