Header Ads

Header ADS

Iran yatoa wito wa watu kubakia majumbani kuepuka Corona

   Idadi ya waliokufa kutokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini Iran imefikia watu 43 na kuwa taifa la pili lenye idadi kubwa ya vifo nje ya China.
Msemaji wa wizara ya Afya ya Iran amearifu kuwa watu 9 wamekufa kutokana na virusi hivyo katika muda wa saa 24 zilizopita na visa maambukizi vimepanda na kufikia watu 593.

Serikali mjini Tehran imeamuru kufungwa kwa shule zote hadi siku ya Jumanne na kurefusha likizo ya vyuo vikuu pamoja na kupiga marufuku matamasha na shughuli za michezo kwa wiki moja.

Maafisa kadhaa wa ngazi ya juu akiwamo makamu wa rais, naibu waziri wa afya na wabunge 5 wamethibitika kuambukizwa virusi hivyo na kuilazimisha serikali kulifunga bunge pamoja na kuweka marufuku ya kusafiri.

No comments

Powered by Blogger.