Header Ads

Header ADS

Rais wa Marekani Donald Trump ameamua kuweka saini ya kuondoa baadhi ya marufuku ya kisheria ambayo mitandao ya kijamii inayo.

Saini hiyo inampa mamlaka ya kuweka hatua za kisheria dhidi ya makampuni ya mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter katika sheria walizoweka katika maudhui wanayochapisha katika mitandao yao.
President Donald Trump
Rais Trump ameishutumu mitandao ya kijamii kwa kushindwa kuwa makini wakati wa kusaini mamlaka ambayo iko huru kuondolewa wakati wa kuweka saini.
Amri hiyo inatarajiwa kukabiliwa na changamoto za kisheria.


Wataalamu wa kisheria wanasema kuwa bunge la Marekani au mfumo wa mahakama lazima iusike ili kubadili sheria iliyopo sasa ambayo inaeleweka kuwa inalinda mitandao ya kijamii.
Rais Trump amekuwa akiishutumu mitandao ya kijamii kila mara kuharihi sauti yake au hat ahata kuweka sauti ambayo hajazungumza lakini anakuwa anasikika kama yeye.
Jumatano, bwana Trump aliishutumu Twitter kwa kuingilia uchaguzi baada ya kuongeza maelezo ya tweet mbili kama uthibitisho.
Alhamisi , Twitter iliongeza taarifa za kuhakiki taarifa kuhusu Covid-19" na kujumuisha ujumbe wa tweet kutoka kwa msemaji wa serikali ya China anayedai kuwa virusi vya corona vilitengenezwa Marekani.

No comments

Powered by Blogger.