Header Ads

Header ADS

Tetesi za Soka Barani Ulaya

           Arsenal inatarajiwa kuanza mazungumzo na wakala wa kiungo wa kati wa Barcelona Phillipe Coutinho.
Mchezaji huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 amehudumia msimu wote akiwa kwa mkopo katika mabingwa hao wa Ujerumani Bayern Munich, lakini klabu hiyo haiko tayari kulipa paundi milioni 105 za Uingereza ili kufanikisha mkataba wa kudumu.(Le10sport - in French).
   Phillipe Coutinho


Paris St-Germain inafanya mazungumzo na Arsenal katika jaribio la kumsaini mashambuliaji wa klabu hiyo Pierre-Emerick Aubameyang, 30, for £34m. (Todofichajes)
Mshambuliaji wa Juventus Gonzalo Higuain, 32, huenda akarudi katika ligi ya premia baada ya uhamisho wake wa mkopo katika klabu ya Chelsea - Newcastle na Wolves zote zinamwania. (Express)
Mshambuliaji wa klabu ya RB Leipzig Timo Werner, 24, amehusishwa pakubwa na uhamisho wa kujiunga na Liverpool lakini aliyekuwa mchezaji wa zamani wa Manchester United Owen Hargreaves anahisi kwamba uhamisho wa klabu hiyo ya Old Trafford ungekuwa bora zaidi kwa mchezaji huyo. (Star)
Mshambuliaji wa Wolves Raul Jimenez, 29 mwenye thamani ya £57m, ananyatiwa na Manchester United, Arsenal na Real Madrid. (Tuttosport - in Italian)

No comments

Powered by Blogger.