Header Ads

Header ADS

Kesi ya Ufisadi inayomkabili rais wa Samani wa Afrika kusini Jacob Zuma yaanza kusikilizwa leo

 Barabara kadhaa zimefungwa karibu na mahakama ya Pietermaritzburg huku kesi ya ufisadi inayomkabili Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma ikiendelea Jumatatu.
Bw Zuma anakabiliwa na mashtaka mengi ya ulaghai na utakatishaji fedha yanayohusiana na mkataba wa silaha wa miaka ya 1990 na kampuni ya Ufaransa.
Anasema mashtaka hayo ni kusaka wachawi na wapinzani wa kisiasa
Julai mwaka jana, maandamano ya ghasia yalizuka katika baadhi ya maeneo ya Afrika Kusini baada ya Bw Zuma kukamatwa katika kesi tofauti.
Changamoto nyingi za kisheria zimesababisha ucheleweshaji wa muda mrefu na kuahirishwa kwa kesi hii inayotarajiwa sana.
Siku ya Jumatatu, mawakili wa Bw Zuma watajibu hati ya kiapo ya mwendesha mashtaka, ambayo inataka kuwasilisha ushahidi mpya.
Pia ametuma ombi la kutaka mahakama kuu iangalie upya rufaa iliyokataliwa mwezi Machi iliyotaka kuondolewa kwa mwendesha mashtaka mkuu akitaja upendeleo.
Rais huyo wa zamani anashutumiwa kwa kupokea pesa katika miaka ya 1990 katika mkataba wa silaha wa $2bn (£1.5bn) na makampuni kadhaa ya Ulaya.
Anashtakiwa pamoja na kampuni ya Ufaransa ya Thales. Wote wanakanusha mashtaka. Bw Zuma pia anakusudia kuendelea na mashtaka ya kibinafsi ya mwendesha mashtaka mkuu.


No comments

Powered by Blogger.