Header Ads

Header ADS

ZUNGU AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA SPIKA WA BUNGE LA WAWAKILISHI LA UFALME WA MOROCCO JIJINI RABAT.

 Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu akizungumza na Spika wa Bunge la Wawakilishi la Ufalme wa Morocco, Mhe. Rachid Talbi Alami katika kikao kilichofanyika leo tarehe 6 Septemba, 2022 katika Ofisi za Bunge hilo Jijini Rabat Nchini Morocco.

Mazungumzo hayo yalijikita kuimarisha Uhusiano wa Kibunge baina ya Mabunge ya nchi hizo pamoja na kuimarisha Ushirikiano wa kiuchumi ikiwemo kilimo.

Mhe. Spika yupo nchini Morocco kwa zaiara ya kikazi ya siku 5.

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu akipokea zawadi kutoka kwa Spika wa Bunge la Wawakilishi la Ufalme wa Morocco, Mhe. Rachid Talbi Alami alipomtembelea leo tarehe 6 Septemba, 2022 Ofisini kwake  Jijini Rabat Nchini Morocco.

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu akiongozana na Spika wa Bunge la Wawakilishi la Ufalme wa Morocco, Mhe. Rachid Talbi Alami baada ya mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 6 Septemba, 2022 katika Ofisi za Bunge hilo Jijini Rabat Nchini Morocco.

Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu akiagana na Spika wa Bunge la Wawakilishi la Ufalme wa Morocco, Mhe. Rachid Talbi Alami baada ya mazungumzo yaliyofanyika leo tarehe 6 Septemba, 2022 katika Ofisi za Bunge hilo Jijini Rabat Nchini Morocco

No comments

Powered by Blogger.