Header Ads

Header ADS

Nabii Jeremia akimuombea muumini wake apate nguvu za kiume nchini kenya

 

Nabii Jeremiah akimuombea muumini wake
Mchungaji mmoja nchini Kenya anayejiita Nabii Jeremiah Kioko, imesambaa video yake mitandaoni ikimuonesha akimuombea mwanaume mmoja ili apate nguvu za kiume kwa kumsukuma kisha kumshika nyeti zake.
Video hiyo imesambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, ambapo Nabii huyo mara baada ya kufanya maombi hayo, muumini wake alisikika akisema tayari nguvu zake zimerejea na kumtaka mke wake ajiandae.
"Ruka juu kwanza achana na nguvu za kiume, nguvu za kiume simamama kuja, mimi naitwa Jeremiah nakupatia nguvu simama, mimi ni transformer wacha nimgawie mtazamaji nasikia ipo kabisa haaa, Bibi yako (mke wako) anakutazama hapa?," aliuliza Nabii Jeremiah
Ambapo mara baada ya maombi hayo muumini huyo alisikika akijibu ,"Nakuja kesho niko chonjo nitakuja ku-kiss na ku-hug,".
Aidha video hiyo pia ipo kwenye akaunti ya TikTok ya mchungaji huyo.

No comments

Powered by Blogger.