Header Ads

Header ADS

Kaimu Katibu Mkuu afanya mazunguzo na Mratibu wa kupambana na usafirishaji haramu wa Binadamu Nchini Marekani


Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Maduhu Kazi (kushoto) akizungumza na Afisa Uratibu wa Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Nchini Marekani, Justin Pollard, jijini Dodoma, leo. Katikati ni Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu nchini, Seperatus Fella. Marekani imeipongeza Tanzania kwa kupanda Daraja (tier 2) kwa kuongeza juhudi ya kupambana na biashara haramu ya usafirishaji binadamu duniani. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu nchini, Seperatus Fella akizungumza na Afisa Uratibu wa Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Nchini Marekani, Justin Pollard (kulia), jijini Dodoma, leo. Katikati ni. Marekani imeipongeza Tanzania kwa kupanda Daraja (tier 2) kutokana na kuonyesha juhudi kubwa ya kupambana na biashara haramu ya usafirishaji binadamu duniani. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Maduhu Kazi (kulia) akimsikiliza Afisa Uratibu wa Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Nchini Marekani, Justin Pollard (katikati), jijini Dodoma, leo, wakati alipokuwa akitoa pongezi kwa Tanzania kwa kupanda Daraja (tier 2) kutokana na kuonyesha juhudi kubwa ya kupambana na biashara haramu ya usafirishaji binadamu duniani. Kushoto ni Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji Binadamu nchini, Seperatus Fella. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


No comments

Powered by Blogger.