Header Ads

Header ADS

Ukraine yadai kupata mafanikio makubwa huku Urusi ikiondoka Kherson

 


Jeshi la Ukraine linasema limepata mafanikio makubwa katika siku ya mwisho karibu na Kherson, baada ya Urusi kusema kuwa inajiondoa katika mji huo wa kusini.
Wanajeshi wa Ukraine wanasema wameukomboa mji muhimu wa Snihurivka, kilomita 50 (maili 30) kaskazini mwa Kherson.
Kyiv pia imedai shinikizo kubwa kwa pande mbili karibu na Kherson, pamoja na kupiga hatua kilomita 7 katika baadhi ya maeneo.
Urusi inasema imeanza kuondoka katika jiji hilo - lakini mchakato huo unaweza kuchukua wiki.
Tangazo la Jumatano lilitazamwa kama kikwazo kikubwa katika juhudi za vita vya Moscow, ijapokuwa maafisa wa Ukraine walikuwa na mashaka - wakionya kwamba ujanja huo unaweza kuwa mtego.
Hakukuwa na ushahidi wa moja kwa moja wa kujiondoa kwa Warusi kwa kiwango kikubwa kutoka Kherson.
Kamanda mkuu wa Ukraine Valeriy Zaluzhny alisema siku ya Alhamisi kwamba hawezi kuthibitisha au kupinga kujiondoa kwa Urusi - lakini akasema majeshi yake yamepiga hatua muhimu.

No comments

Powered by Blogger.