Header Ads

Header ADS

Naibu waziri amezindua zoezi la utafiti wa gharama za utapiamlo nchini

           

 Pichani ni Naibu Waziri Ofisi Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa zoezi la utafiti wa Gharama za utapiamlo nchini zoezi lililofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma.

 Pichani niMwakilishi Mkazi  Nchini wa Shirika la Mpango wa  Chakula Duniani (WFP) Bi, Sara Gibson  akitoa neno la utangulizi katika hafla ya uzinduzi wa zoezi la utafiti wa Gharama za utapiamlo nchini zoezi lizoezi lilofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome Jijini Dodoma. 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amezindua Rasmi zoezi la utafiti wa gharama za Utapiamlo nchini, ikiwa ni sehemu ya  utekelezaji wa maazimio ya viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kupitia mpango ujulikanao kama “The Cost of Hunger Study in Africa – COHA” ambapo Mheshimiwa DKt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameridhia ufanyike ikiwa ni  nia yake ya dhati ya kuondoa utapiamlo nchini.

 Aidha,uzinduzi huo Uliofanyika katika Ofisi wa Waziri Mkuu Jijini Dodoma . Naibu Waziri Nderiananga Alisema, Lengo la utafiti ni kubainisha makadirio ya gharama zinazosababishwa na matatizo ya lishe duni yani utapiamlo kijamii na kiuchumi na hususan katika nyanja za sekta ya afya, elimu na nguvu kazi. 

Aliongezea kuwa Tanzania itakuwa nchi ya 22 Barani Afrika kufanya utafiti kama huo pindi utakapokamilika na  kwa mwaka 2024, takribani nchi 6 (ikiwemo Tanzania) zimeonesha utayari wa kufanya utafiti huo ili kuwezesha nchi kupanga malengo ya kupunguza upotevu wa pato itokanayo na utapiamlo na kuwekeza katika maeneo ya maendeleo.

vile vile, Naibu Waziri Nderiananga  amewashukuru wataalamu wa Chakula na Lishe kwa kuishauri vyema Serikali juu ya umuhimu wa utafiti katika nchini.


“Tunapokwenda kuandaa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050, niwashukuru wadau wetu wakiwemo Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF) ambao tayari wameshatoa fedha ambazo zitasaidia sana katika hatua muhimu za utafiti huu”. Alisisita

Kwa upande wake Mwakilishi  kutoka UNICEF Bw. John George ametoa pongezi kwa Serikali kwa kujiunga na Mpango wa COHA na kutambua nafasi ya mtoto ambaye ndiye mlengwa mkubwa katika mpango huo na kwa tafiti zilizotoa takwimu za utapiamlo nchini.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mwakilishi Mkazi Nchini, wa Progamu ya Chakula Duniani (WFP) Bi Sarah Gibson Alisema Tafiti hizo zitasaidia kukabiliana na madhara yatokanayo na Utapiamlo nchini kama vile ukuaji kwa mtoto na huweza kuleta athari katika elimu ya mtoto na Maendeleo ya Taifa kwa Ujumla.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw.Salihina Ameir amesema kwa Upande wa Zanzibar, Ofisi hiyo ina nafasi kubwa katika Uratibu wa masuala ya Kiuchumi kisiasa na Kijamii ikiwa ni Pamoja na masula ya Tafiti za Lishe.

Hata hivyo,zoezi zima la uzinduzi wa gharama za zoezi la Tafiti za Utapiamlo nchini, linafadhiliwa na Programu ya Chakula Duniani (WFP) pamoja na  wadau wengine wa maendeleo nchini kama vile USAID, FAO, Irish Embassy, Hellen Keller International – HKI na UNICEF

No comments

Powered by Blogger.