Header Ads

Header ADS

Mafuta yapanda bei kutokana na mashambulio dhidi ya Vituo vya Mafuta Saudia

    Gharama ya mafuta imepanda kwa kiwango cha juu kuwahi kushuhudiwa katika miezi minne baada ya mashambulio mawili dhidi ya vituo vya mafuta Saudi Arabia Jumamosi yaliosababisha kumwagika kwa 5% ya mafuta duniani.
Kiwango cha mafuta ghafi yalipanda kwa 19% kwa thamani ya $71.95 kila mtungi huku viwango vingine, West Texas Intermediate, vikipanda 15% kwa thamani ya $63.34.
Bei zilishuka kidogo baada ya rais wa Marekani Donald Trump kuagiza kufunguliwa kwa akiba nchini Marekani.
Smoke is seen following a fire at Aramco facility in the eastern city of Abqaiq
Huenda ikachukua wiki kadhaa kabla ya vituo hivyo Saudia kurudi katika hali ya kawaida.
Mashambulio hayo dhidi ya vinu katika shina la viwanda vya mafuta saudia vinajumuisha kituo kikubwa duniani cha usafishaji mafuta.
Fire at Saudi oil facilityHaki miliki ya pichaS
Image captionMoto uliozuka katika kituo cha mafuta Saudia mwishoni mwa juma
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amesema Tehran imehusika na mashambulio hayo. Iran imeishutumy Marekani kwa 'uongo'.
Baadaye Trump amesema katika ujumbe wa Twitter kuwa Marekani inafahamu mhusika wa uhalifu huo ni nani na ipo tayari ila inasubiri kusikia kauli ya WaSaudi kuhusu namna ambavyo inataka kulifuatilia hili.
Katika ujumbe mwingine kwenye twitter, amesema " kuna mafuta mengi!".
Athari yake kwa usambazaji mafuta ni ipi?
Wasaudi hawajaeleza kwa kina kuhusu mashambulio hayo, kando na kusema kwamba hakuna aliyeathirika, lakini imetoa ishara kidogo kuhusu utengenezaji mafuta.
Waziri wa nishati mwanamfalme Abdulaziz bin Salman amesema kupungua kwa utengenezaji mafuta kutafidiwa kwa kutumia akiba kubwa iliopo.
Ufalme huo ndio wauzaji wakuu wa mafuta duniani, ambapo unasafirisha zaidi ya mitungo milioni 7 kwa siku ya mafuta.
"Maafisa wa Saudia wamedai kudhibiti moto huo, lakini sio kuwa umezimwa kikamilifu," amesema Abhishek Kumar, mkuu wa takwimu katika shirika la Interfax Energy mjini London. "Uharibifu kwa vituo vya Abqaiq na Khurais unaonekana kuwa mkubwa, na huenda ikachukua wiki kadhaa kabla ya usambazaji mafuta ukarudi katika hali ya kawaida."
Saudi Arabia inatarajiwa kutumia akiba ili usafirishaji mafuta uendelee kama kawaida wiki hii.

Hatahivyo, Michael Tran, mkurugenzi msimamizi wa mipango ya nishati katika soko la RBC Capital Markets mjini New York, amesema: "hata iwapo tatizo hilo litatatukiwa kwa haraka, tishio la kutenga 6% ya mafuta yanayotengenezwa duniani sio fikra tu. Kutahitajika, faida ya ziada inayohitajika kwa mwekezaji kujilipa."

No comments

Powered by Blogger.