Header Ads

Header ADS

Abiria Zaidi Ya Hamsini Wanusurika Kifo Kufuatia Kupasuka Kwa Tairi La Mbele La Basi

  Abiria zaidi ya 50 waliokuwa wakisafiri kutoka Mbeya kuelekea mkoani Songea wamenusurika kufa baada ya basi lao aina ya Huger la Kampuni ya Superfeo lenye namba ya usajili T885 DJS kupasuka tairi ya kushoto na hivyo kuacha njia na kuingia porini katika Kijiji cha Mkongotema Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma.

Aidha,Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana lakini uchunguzi bado unaendelea.

No comments

Powered by Blogger.