Header Ads

Header ADS

Chama cha ACT.Wazalendo Mkoa wa Njombechafungua dirisha la uchukuaji fomu za Uchaguzi Serikali za Mitaa 2019

    Katibu mwenezi wa Chama cha ACT Mkoani Njombe Stanley.E.Mbermbati amewakumbusha Wanachama wa ACT Mkoani humo kuwa fomu za wagombea katika uchaguzi wa Serikali za mitaa zimeanza kutolewa maeneo mbalimbali ya Mkoa huo pia kwa mgombea yeyote atakae itaji fomu hiyo afike katika Ofisi ya Jimbo anakotokea.         
Image result for ACT WAZALENDO NJOMBE
    Aidha,Stanley ameendelea kueleza kuwa kwa wale ambao wanaitaji kadi ofisi zote za Majimbo na matawi zipo wazi kwa ajili yao.
 "Natoa wito kwa tume ya uchaguzi,simamieni haki,wapeni uhuru watanzania wachague viongozi wanaowataka ili wapate hamasa ya kuendelea kushiriki chaguzi nyingine zijazo''.Amesema Mbembati
   Hata hivyo,ameendelea kusema kuwa''ACT Wazalendo tumedhamilia kushinda uchaguzi wa mitaa na vijiji vyote hatimaye uchaguzi mkuu hapo mwaakani''.
  Lakini pia,amewaomba watanzania waungane na chama hicho kwani Serikali ya wanyonge imewaacha na unyonge kwenye kilimo,mifugo,sekta ya elimu,wafanya biashara nk.
  ''Watanzania  chagueni viongozi wa upinzani  msirudia tena makosa yaleyale kwani CCM ni ileile msidanganyike kuwa kuna CCM mpya na ya zamani.Lakini mwisho amewatakia watanzania maandalizi mema ya uchaguzi''.Amesema Stanley
  Hali kadharika amesema kuwa kwa wale wanachama wanaoitaji kadi hizo wanaweza kuwasilia kupitia namba ya simu ya Katibu Mwenezi Mkoa +22763934944.
     

No comments

Powered by Blogger.