Header Ads

Header ADS

Dkt, Ndugulile amewaagiza Wataalamu wa Sekta ya Afya nchini kuwekeza katika kufanya tafiti.

    Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza Wataalamu wa Sekta ya Afya nchini kuwekeza katika kufanya tafiti ili kutatua changamoto za Magonjwa yasiyoambukiza nchini.
    Ameyasema hayo leo wakati akifungua Kongamano la Kwanza la Kitaifa Kuhusu Udhibiti wa Magonjwa Yasiyoambukiza, lililohudhuriwa na Wataalamu mbali mbali wa masuala ya Afya, katika ukumbi wa chou cha UDOM, Jijini Dodoma.


  Pia, Dkt Ndugulile amesema kuwa, Licha ya kuwa na tafiti mbali mbali za Magonjwa yasiyoambukiza, bado kuna haja yakufanya tafiti zakutosha, ili kuendana na kasi ya matatizo ya magonjwa haya ambayo yanazidi kuwa tishio katika jamii yet una Dunia kwa ujumla.
 “Tunapoanza mpango huu, mimi niwaombe sana Wanazuoni na Wanataaluma wengine tuwekeze kwenye tafiti, mpango huu hautakuwa na maana, kama hatukuwa na takwimu, zitazosaidia kujua kama tunapiga hatua au la”, amesema Dkt. Ndugulile
  Aidha, Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Grace Magembe amesema Alisema, awali Serikali ilijikita katika kukabili magonjwa ya kuambukiza kama vile malaria, kifua kikuu, ukimwi na mengineyo lakini sasa hali inaonesha kasi ya magonjwa yasiyoambukiza ni kubwa.
   Pia, Dkt. Maghembe amesema, gharama za matibabu dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza unazidi kuielemea jamii na Serikali, huku akidai kuwa, Magonjwa yasiyoambukiza yanachukua zaidi ya asilimia 40 ya bajeti ya sekta ya afya.
   Hata hivyo,aliendelea kusema, “Bajeti yetu yote ya afya inaingia kwenye magonjwa haya, ni gharama kubwa kuyatibu, kuanzia ugunduzi, dawa, vifaa tiba ni ghali, kuyatibu ni tofauti na yale ya kuambukiza.

No comments

Powered by Blogger.