Header Ads

Header ADS

Watu sita wafikishwa mahakamani na TAKUKURU

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU wilayani Igunga  mkoa wa Tabora imewakamata viongozi sita wa chama cha Msingi cha Wakulima wa zao la pamba AMCOS wa kijiji cha Choma na kuwafikisha mahakama ya hakimu Mfawidhi wilaya ya Igunga kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa kutoka kwa wakulima.

    Kwa upande wa muendesha mashitaka wa taasisi hiyo Mazengo Joseph aliiambia mahakama mbele ya hakimu Lydia Ilunda kuwa washitakiwa wote walitenda makosa hayo kinyume na kifungu cha 15 (1) a (2) na 3 (a)  sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa na 11 ya 2007.
       Waliofikishwa Mahakamani mwisho wa wiki hii iliyopita ni Mwenyekiti wa baumu  AMCOS , Nyolobi Nangale (36), Sylvester Masanyigule (46), Andrew Senga(49), Iwize Masanja(37) Elias Kelege (25), Martine Silas (31) wote wakiwa ni wakazi wa kijiji cha choma

 
Muendesha mashitaka Mazengo Joseph amesema kuwa washitakiwa wote wanakabiliwa na mashitaka matatu shitaka la kwanza, kati ya agosti 1 mwaka huu na Oktoba 25 mwaka huu kwa muda tofauti katika kijiji cha choma, washitakiwa wote kwa pamoja waliomba rushwa ya shilingi laki nane kutokea kwa Kulwa Mabula ili waweze kumlipa fedha zake za pamba shilingi milioni nane laki tatu arobaini na tano elfu miambili Ishirini alizokuwa ameiuzia pamba kampuni ya OLAM.
Shitaka la pili linalowakabili washitakiwa wote katika tarehe hiyo na muda tofauti waliomba rushwa ya shilingi laki sita kutoka kwa Shimbi Ganja ili waweze kumlipa fedha zake shilingi 6,536,400 alizokuwa ameuza pamba kwenye kampuni ya OLAM.
Shitaka la tatu amesema katika tarehe hiyo na muda tofauti waliomba rushwa ya Shilingi laki sita kutoka kwa Shimbi Kadengu ili waweze kumlipa fedha zake Shilingi milioni 6,220,680 aliyouza pamba kwa kampuni ya OLAM.
Hata hivyo baada ya kusomewa mashitaka hayo waliyakana yote ambapo kesi hiyo imehairushwa hadi novemba 6 mwaka huu itakapotajwa tena ambapo washitakiwa wawili wamedhaminiwa kwa dhamana ya shilingi milioni  tano mmoja huku wanne wakipelekwa mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

No comments

Powered by Blogger.