Header Ads

Header ADS

Chadema wahakikisha kushinda na kuliongoza Jiji la Dodoma mwaka huu.

 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA]kanda ya kati,Lazaro Nyalandu amesema katika mwaka huu wa Uchaguzi mkuu,2020 Chama hicho kimejipanga kushinda na kuliongoza jiji la Dodoma.
 Akizungumza leo Januari,12,2020 jijini Dodoma na Waandishi wa habari Mhe.Nyalandu amesema Kipaumbele cha  CHADEMA kanda ya kati ni kuhakikisha jiji la Dodoma linakuwa mikononi mwa Chama hicho.

"Kipaumbe No 1 cha CHADEMA kanda ya kati ambapo mimi naongoza ni kuhakikisha tunaliongoza  jiji la Dodoma,ambalo ni makao makuu ya nchi yetu kama ilivyo desturi ya CHADEMA ni kuchukua kwanza eneo ambalo watawala wamekaa.Kama mnakumbuka mwaka 2015 jiji la Dar Es Salaam lilichukuliwa na CHADEMA"amesema.
 Hata hivyo,ameendelea kusema "Tutashinda kwa mbinu zinazojulikana na mbinu zisizo julikana hivyo Wanachama tuhakikishe tunaipa raha CHADEMA"ameeleza Nyalandu.
 Aidha, Mwenyekiti huyo wa CHADEMA kanda ya Kati amesema kuna uhitaji mkubwa wa kuwa na tume huru ya Uchaguzi hali itakayoipa heshima Kubwa nchi ya Tanzania  na Kuisaidia CCM itakapokuwa Chama cha Upinzani.
 "Kuna Msisitizo mkubwa sana ambapo pana uhitaji wa tume huru ya uchaguzi ,Demokrasia yetu itakuwa ya kuigwa Afrika Mashariki na ukanda wa SADC kwa ujumla"amesema Nyalandu.
 Katika hatua nyingine Nyalandu amesema  mchakato wa kurekebisha daftari  la Mpiga kura lifanyike kwa ueledi kabla ya uchaguzi huku akiomba sheria ya vyama vya siasa kufanyiwa marekebisho hali itakayoruhusu wanasiasa  na asasi za kiraia kuruhusiwa  kushiriki kuhamasisha watu kujiandikisha kwenye daftari la mpiga kura huku pia akisisitiza vyombo vya Ulinzi na Usalama kutojihusisha na Masuala ya siasa.
 Mbali na hayo Nyalandu amesema CHADEMA sio chama cha kulalamika tu na kuwaomba wanaohusika na Masuala ya kilimo kuhakikisha wanasambaza pembejeo za kilimo katika kipindi hiki cha  Mvua ili wakulima walime kwa wakati hali itakayosaidia kupata chakula cha kutosha.

No comments

Powered by Blogger.