Header Ads

Header ADS

Waziri wa elimu wa Uganda Janeth Mseveni apewa wito wa kufika bungeni

  Spika wa bunge la uganda ametoa wito kwa mke wa rais wa Uganda ambaye  ni Waziri wa Elimu, Janet Museveni kufika mbele ya chombo hicho cha kutunga sheria kufuatia mkanganyiko kuhusu kuanza kutumika kwa mtaala mpya wa elimu.

  Waziri huyo alishindwa kufika mbele ya bunge Jumanne Februari 18 mwaka huu kufuatia wito uliotolewa na Spika Rebecca Kadaga wiki iliyopita.

  Sanjari ya  kushindwa kufika alituma udhuru kupitia kwa Waziri wa Elimu ya Msingi, Rosemary Seninde, akiomba kuitikia wito huo Februari 20, 2020.
  Aidha, spika ametoa wito wa mwisho na kusema kwamba kiongozi huyo ana nafasi moja ya mwisho.
  Kwa mujibu wabunge nchini Uganda wanaituhumu wizara hiyo kuanza kutumia mtaala mpya kwa  wanafunzi wa elimu ya sekondari licha ya bunge kuamuru kusitishwa mpango huo. Wabunge walizuia mtaala huo kuanza kutumika kutokana na upungufu wa vitabu, na upungufu wa waalimu wenye ujuzi wa kutumia mtaala huo.

No comments

Powered by Blogger.