Header Ads

Header ADS

Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Malala afunga ndoa

 Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Malala Yousafzai "amefunga pingu za maisha" na mpenzi wake wakati wa sherehe za Kiislamu huko Birmingham.

Yeye na Asser Malik walishiriki katika sherehe ya nikkah, ambapo bibi na bwana harusi wanaruhusiwa kuoana.

Mwanaharakati huyo mwenye umri wa miaka 24 alisema ilikuwa "siku ya thamani" katika maisha yake.

Mwanaharakati huyo wa haki za wanawake wa Pakistan alipata hifadhi Magharibi mwa Midlands baada ya kupigwa risasi kichwani na Taliban mwaka 2012.

"Mimi na Asser tumefunga pingu za maisha kuwa wenzi wa maisha," aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter Jumanne, akielezea jinsi walivyoshiriki katika "sherehe ndogo ya nikkah na familia.

"Tuna furaha sana kuanza pamoja safari hii iliyo mbele yetu," aliongeza

Malala, ambaye sasa ana umri wa miaka 24, alikuwa na umri wa miaka 15 alipolengwa na Taliban nchini Pakistan alipozungumza kutetea haki ya wasichana kupata elimu.

Alinusurika katika shambulio hilo, ambapo mwanamgambo alipanda basi lake la shule kaskazini-magharibi mwa bonde la Swat na kufyatua risasi, na kuwajeruhi marafiki zake wawili wa shule pamoja na yeye mwenyewe Malala.

Baada ya kupona majeraha, yeye na familia yake walihamia Birmingham, ambako baadae alikuita nyumbani kwake kwa pili.

Katika umri wa miaka 17, alikuwa kijana mdogo kupata ushindi wa tuzo ya amani ya Nobel. Alienda kusoma chuo kikuu cha Oxford, na kuwa kinara wa kampeni za kutetea haki za binadamu.


No comments

Powered by Blogger.