Header Ads

Header ADS

UN :yaishutumu Ethiopia kwa kuwashikilia wafanyakazi wake

 Umoja wa Mataifa umesema wafanyakazi wake 16 wamezuiwa katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa alisema wengine sita wameachiliwa huru.

Alisema Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo imetakiwa kuwaachilia wote mara moja.

Bado haijabainika kwanini walikamatwa. Mwezi uliopita maafisa saba wakuu wa Umoja wa Mataifa walifukuzwa baada ya kushutumiwa kuingilia masuala ya Ethiopia.

Umoja wa Mataifa umezungumza kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu na umeishutumu serikali kwa kuzuia utoaji wa misaada kwa mamilioni ya waathirika wa mgogoro kaskazini mwa Ethiopia.

Kumekuwa na shutuma nyingi kwamba watu wa Tigray wamekamatwa kiholela - jambo ambalo serikali inakanusha.



No comments

Powered by Blogger.