Header Ads

Header ADS

Mahakama yapiga marufuku Polisi ambao hawajaolewa kupata ujauzito

 Mahakama Kuu nchini Nigeria imedumisha uamuzi wa kikosi cha polisi kumfuta kazi afisa wa polisi wa kike ambaye alipata ujauzito nje ya ndoa mwaka jana.
Jaji Inyang Ekwo alisema hakuona sababu ya kutosha "kuvuruga nidhamu ya jeshi".
"Mtu yeyote anayejiunga na jeshi lazima azingatie kanuni za jeshi au asijiunge na jeshi kwani hakuna sio lazima," aliongeza.

Kesi hiyo iliwasilishwa mahakamani na Chama cha Wanasheria wa Nigeria kufuatia kufutwa kazi kwa afisa ambaye hajaolewa ambaye alipata ujauzito Januari 2021.
"Maafisa wa polisi wa kiume na maafisa wa polisi waliooa katika Jeshi la Polisi la Nigeria hawabaguliwi, kuwekewa vikwazo, kuonewa na kudhalilishwa hivyo," ilisema.


No comments

Powered by Blogger.