Header Ads

Header ADS

Jeshi la polisi mkoani Mbeya lakamata pombe zilizopigwa zilizokatazwa Tanzania

 

Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya limefanikiwa kumkamata mtu mmoja akiwa na pombe kali zilizopigwa marufuku nchini.

Katika taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Ulrich Matei imesema ,mtuhumiwa huyo anafahamika kwa jina la Ishengoma Peter Kaswela (36)Mkazi wa Ndandalo alikamatwa Mnamo tarehe 18.06.2022 majira ya saa 11:00 jioni, akiwa na pombe kali zilizopigwa marufuku nchini zikitokea nchi jirani ya Malawi ambazo ni Ice Dry London Gin box 01 na Coferhum box 05 ambazo ni sawa na chupa 120. 

Kamanda amesema alikamatwa wakati jeshi la polisi likiwa kwenye huko Kasumulu Kitongoji cha Seko, Kijiji na Kata ya Njisi, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya.

Aidha Matei amesema mtuhumiwa ni muingizaji wa bidhaa za magendo na muuzaji wa pombe hizo.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu katika maeneo mawiwi tofauti wakiwa na Pombe haramu ya Moshi (Gongo).

 

Watuhumiwa wawili wa kwanza ni Hawa Kapangala (40) mkazi wa Kiwira na Emanuel Edwin Mwakajela (50) mkazi wa Kiwira  ambao  walikamatwa mnamo  tarehe 17.06.2022 majira ya saaa 06:45 mchana katika  Kitongoji cha Kiwira kati, kijiji cha Mpandapanda, kata ya Kiwira, tarafa ya Ukukwe,wilayani Rungwe.

 

Pia katika kitongoji cha Mshikamano, Kata ya Nsalala, Tarafa ya Usongwe, Mkoa wa Mbeya mnamo 18.06.2022 majira ya saa 05:00 asubuhi, jeshi la polisi lilifanikiwa kumkamata Yunice Geofrey Mwakifwamba [40] mkazi wa Mshikamano, akiwa na Pombe Haramu ya Moshi lita 15 akiwa amehifadhi katika madumu mawili ya lita 5 na chupa za maji nne zenye ujazo wa lita 1.5 zikiwa na kuzificha uvunguni mwa kitanda.

 

Watuhumiwa wote ni wauzaji wa Pombe hiyo na watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi wa mashauri yao kukamilika.

 

No comments

Powered by Blogger.