Header Ads

Header ADS

Serikali Tabora kupambana na vitendo vya ukatili kwa watoto

Serikali Mkoani Tabora imesema itahikikisha inapambana vikali kuzuia vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto wadogo ndani ya mkoa huo.

Mkuu wa wilaya ya  Nzega  kamishina msaidizi wa polisi Advera  Bulimba akitoa zawadi kwa mmoja ya wanafunzi walionda tuzo ya uandishi wa Insha iliyohusu mimba na ndoa za utotoni

Hayo yamezungumzwa ikiwa tatizo la ukatili wa kijinsia ,mimba na ndoa za utotoni likitajwa  kushika kasi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tabora ambapo serikali imetaja kuongeza makali ya kusimamia sheria kwa wale wanaokamatwa na tuhuma za kuvunja matakwa ya haki za watoto .

Mkuu wa wilaya ya  Nzega  kamishina msaidizi wa polisi Advera  Bulimba  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora  balozi Dkt. Batilda Buriani katika  hafla fupi ya kuwapongeza wanafunzi walioshinda shindano la uandishi wa insha kuhusu ukatili na kupinga mimba na ndoa za utotoni.

Alisema kwamba serikali haina lelemama na wale ambao wamekuwa wakifanya vitendo vya hovyo kwa watoto.

Mkuu huyo wa wilaya  aliendelea kusema kwamba serikali ya mkoa wa Tabora itapingana kuhakikisha  Ukatili dhidi  matendo ya ubakaji, ulawiti, utumikishwaji wa watoto, kunyimwa haki ya elimu, vipigo, kutopatiwa mahitaji ya msingi au kutelekezwa pale wazazi wanapotengana, kudhulumiwa mirathi na walezi vinakomeshwa ili kuweza kumlinda motto huyo.

“Wazazi wanapofariki,watoto wa kike kulazimishwa kuolewa katika umri mdogo na mimba za utotoni jambo ambalo linakera sana kwani sio haki kwa mtoto kupitria madhira hayo” alisema Advera  Bulimba  

ACP Advera  Bulimba   alisema kwamba serikali itaendelea kuhamasisha na  kusimamia utekelezaji wa sheria, kanuni na miongozo  ili kuhakikisha adhma ya kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya ukatili inatekelezeka kwa vitendo.

 Akizungumza kwa niaba ya mkurungezi wa shirika la World Vision Esther Mongi alisema kwamba  Mtoto aliyefanyiwa  vitendo kikatili  anaweza kupata madhara ya kisaikolojia, kimwili na kitabia, pia kuathiri mwenendo mzima wa  malezi na makuzi, kujifunza na mahusiano yake na jamii hapo  baadaye atakapokuwa mtu mzima kwa kuendelea kuamini  kuwa ukatili ni sehemu ya maisha.

Alisema kwamba Vitendo vya ukiukwaji wa haki za Watoto hufanywa na wazazi, walezi, ndugu waliopo katika familia, Watoto kwa Watoto, wanajamii kwa kuwapatia watoto kazi ngumu na kuwafanyia ukatili kutokana na umaskini .

Aliendelea kusema kwamba  baadhi ya watendaji wa Serikali,  wafanyakazi katika mashirika yasiyokuwa ya serikali, na wamiliki wa migodi na Wafanyabiashara.

Alisisitiza kwamba shirika la World Vision litaendelea kupambana na mila na desturi, mabadiliko ya sayansi na teknolojia navyo vimeendelea kuwa ni visababishi vya matendo ya ukatili kwa Watoto.

Aidha kaimu mkurungezi  huyo alisema kwamba  shirika la World Vision Esther Mongi litaendelea   kuwajengea uwezo watoto ili waweze  kujiamini na kujitambua ikiwa hatua ya kukabiliana  na tatizo la  mimba na ndoa za utotoni .

Alisema kwamba shirika hilo linaendelea  kuratibu  mashindano ya  uandishi wa insha  kwa  wanafunzi wa shule za msingi ambapo katika Mkoa wa Tabora  washindi wamepewa  zawadi za baiskeli na fedha tasilimu huku   mshindi wa kwanza kwa mkoa wa Tabora akitarajiwa  hivi karibuni kwenda  kushiriki mashindano hayo kitaifa Mkoani  Dodoma.

Afisa maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya  ya Nzega Robert Mwanga alisema  jamii inatakiwa kuwa sehemu ya kuwalinda watoto huku  watoto wenyewe wakiombwa  kuwa ni sehemu  ya kutoa taarifa  pale wanapokumbana na viashiria  vya uvunjifu wa haki zao.

Mkuu wa wilaya ya  Nzega  kamishina msaidizi wa polisi Advera  Bulimba akitoa zawadi kwa mmoja ya wanafunzi walionda tuzo ya uandishi wa Insha iliyohusu mimba na ndoa za utotoni


No comments

Powered by Blogger.