Header Ads

Header ADS

Jimbo la Singida Mashariki la ahidiwa na Rais John Magufuli kutekeleza miradi ya maji.

    Kwa mujibu wa Rais John Magufuli ameeleza kuwa jimbo la Singida Mashariki lilitelekezwa pasipo kuwepo na mwakilishi wa mbunge.
    Tundu Lissu,ambaye aliyepewa dhamana ya kuliongoza jimbo la Singida Mashariki kupitia tiketi ya chama pinzani CHADEMA kwa hawamu ya pili mwaka 2015,lakini toka septemba 7,2017 mbunge uyo alikuwa nje ya Tanzania kwa ajili ya matibabu mara baada ya kushambuliwa kwa kupigwa lisasi na watu wasiojulikana.
    Na kupelekea jimbo hilo kuwa bila kuwepo kwa mwakilishi bungeni katika kipindi chote hicho.











  "Saa nyengine majimbo yanakosa uwakilishi...Kama ulivyoagiza mheshimiwa Spika (Job Ndugai)kwamba tushughulikie tatizo la maji katika jimbo lile…kama tulivyoshughulikia jimbo la Dar es Salaam…ninakuahidi kwamba serikali yangu itashughulikia, ili yale yaliyokuwa yamechelewa yaanze kufika haraka haraka," amesema Magufuli.
Amesema wote wanaojaribu kubeza ama kuzuia Shirika la Ndege la Nchi hiyo (ATCL) hawatafika popote na kudai wanayoyafanya ni sawa na "kelele za chura."
"Mkiona watu wanakamata ndege yetu msishangae. Kwa sabubu shirika letu linafanya vizuri."
Magufuli pia amejaribu kutumia mashairi ya kibao cha Extravaganza cha bendi ya Suti Sol ya Kenya: "...wakifunika, tunafungua...hawazuiliwa kufanya kitu. Wakiwafungia kuingia ndani, wanawakuta wapo ndani. Sasa sisi ni hivyo hivyo. Wajijaribu hivi, tutafanya hivi. Wakifanya hivi tutafanya hivi.Ili nchi yetu iendelee mpaka ifike tunapopanga."

No comments

Powered by Blogger.