Header Ads

Header ADS

Wanafunzi saba wafariki Dunia na wengine wajeruhiwa

Wanafunzi saba wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya jengo la darasa la Shule ya Precious Talent kuanguka eneo la Ngado Nairobi nchini Kenya saa 1 asubuhi leo Jumatatu Septemba 23, 2019. 

Shule hiyo ipo mkabala na Barabara ya Ngong'; shughuli za uokozi zinaendelea kwa sasa huku ikiarifiwa tayari 
wanafunzi zaidi ya 50 wametolewa kwenye vifusi na kupelekwa Hospitali Kuu ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH). 
Wanafunzi saba wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa baada ya jengo la darasa la Shule ya Precious Talent kuanguka eneo la Ngado Nairobi nchini Kenya saa 1 asubuhi leo Jumatatu Septemba 23, 2019. 

Shule hiyo ipo mkabala na Barabara ya Ngong'; shughuli za uokozi zinaendelea kwa sasa huku ikiarifiwa tayari wanafunzi zaidi ya 50 wametolewa kwenye vifusi na kupelekwa Hospitali Kuu ya Kitaifa ya Kenyatta (KNH). 

Kwa Mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya shughuli ya uokoaji inaendelea na wanafunzi wanne wamepelekwa Hospitali ya Taifa ya Kenyatta.

Kamanda wa polisi George Seda na mbunge wa eneo la Dagoreti, John Kiarie, wamethibitisha kuongezeka kwa idadi ya vifo kutokana na ajali hiyo.

Mkurungezi wa shule hiyo ya kibinafsi, Moses Wainaina Ndirangu, amaeiambia Runinga ya Citizen nchini Kenya kuwa jengo hilo liliathiriwa na ujenzi wa bomba la maji taka karibu unaoendelea karibu na hapo.

Baadhi ya wanafunzi wanasemekana kukiimbilia makaazi ya watu walio karibu na mtaa waDagoretti, Magharibi mwa Jiji la Nairobi baada ya jengo la shule kuporomoka.

No comments

Powered by Blogger.