Header Ads

Header ADS

Raisi wa Urusi, Vladmir Putin amesema kuwa nchi yake inaweza kuisaidia Afrika bila masharti ambayo huambatanishwa kwenye misaada ya mataifa ya magharibi.

Raisi wa Urusi, Vladmir Putin amesema kuwa nchi yake inaweza kuisaidia Afrika bila masharti ambayo huambatanishwa kwenye misaada ya mataifa ya magharibi.
''Tunaona jinsi mataifa ya magharibi yanavyotoa mashinikizo na vitisho dhidi ya serikali huru za kiafrika,'' Putin ameeleza katika mahojiano na shirika la habari la Urusi TASS, kabla ya mkutano na viongozi wa Afrika.
''Wanatumia njia hizo ili kurejesha nguvu ya ushawishi na utawala kwenye makoloni yao ya zamani na kulinyonya bara la Afrika,'' aliongeza.
Vladmir Putin ana mipango kabambe kwa Afrika?
Urusi inatarajia kuwa mwenyeji wa viongozi 47 wa Afrika katika mkutano wa tarehe 23 -24 mwezi Oktoba mjini Sochi.
Bwana Putin amesema mahusiano na Afrika yemeimarika, akiainisha makubaliano ya ushirikiano katika masuala ya silaha, ambapo Urusi imefanikiwa kushawishi mataifa zaidi ya 30 kuwasambazia silaha.
Rwanda ni moja ya nchi ambazo zimekuwa na mahusiano mazuri sana na Urusi
Baraza la mawaziri la Rwanda hivi karibuni liliridhia makubaliano na urusi katika masuala ya matumizi ya nishati ya nyukilia kwa ''matumizi ya amani'',Gazeti la The East Africa limeripoti.

Teknolojia hii itatumika katika uzalishaji wa nishati na utunzaji wa mazingira, ripoti imeeleza.
arekani imekuwa chanzo kikubwa cha uwekezaji wa moja kwa moja barani Afrika, lakini mchango wake umekuwa ukipungua.
Mwaka 2018, China ilitangaza uwekezaji wa thamani ya dola za kimarekani bilioni 60 kwa ajili ya miradi ya miundombinu.
Bi Benabdallah amesema kuwa biashara kati ya Marekani na mataifa ya Afrika imeshuka kwa sababu ya ongezeko la uhitaji si tu China,lakini nchi nyingine kama vile Urusi na Uturuki.
''Nafikiri ni kwa sababu ushindani kutoka kwa nchi nyingine umeongezeka katika kipindi cha muongo mmoja uliopita,'' amesema bi Benabdallah.
Ukuaji wa uchumi wa China umeonyesha dalili za kushuka hivi karibuni, hali ambayo itaathiri biashara na uwekezaji katika Afrika siku za usoni.
Lakini kutokana na ushindani kutoka duniani kote kwa kufanya biashara na nchi za kiafrika, Marekani inapambana kurejesha mahusiano na bara la Afrika kwa kujihusisha na nchi za uchumi unaochipukia.

No comments

Powered by Blogger.