Header Ads

Header ADS

Wasio Oa na kuolewa kucharazwa bakola

   Albert Chalamila mkuu wa mkoa wa Mbeya ameeleza kuwa ana mpango mpya ambao utahusisha na kucharaza fimbo kwa wale wanawake wasio olewa pamoja na wanaume wasio oa mkoani humo pia mara baada ya kumaliza kuwachalza viboko atawaagiza waende wakatafute wapenzi wao ambao wa kufunga nao ndoa.
   Hayo amezungumza mkoani humo ambapo ameeleza kwamba njia ya kutumia bakora ni njia pekee ambayo inaweza kuhamasisha jambo kwa haraka zaidi kuliko njia zingine.











    "Siku hizi tunatumia bakora katika kila jambo, tukikukuta umekaa nyumbani na huolewi ni bakora tu nenda katafute mume na ukiwa umekaa nyumbani huoi ni bakora tu nenda katafute mke, kuna umri ambao unatosha lazima uchangamshwe'' amesema Chalamila.
    Aidha,vyombo mbalimbali vya habari vilitawala habari za mkuu wa mkoa huyo zikionyesha anawachalaza viboko baadhi ya wanafunzi wanaosadikika kuhusika na uteketezaji wa mabweni ya shule ya Sekondari kiwanja iliyopo Wilayani Chunya.
     Imeripotiwa na mwandishi wetu;Adolf Mwingira.

No comments

Powered by Blogger.