Header Ads

Header ADS

Waziri awataka wamiliki wa viwanda kuboresha utendaji wao.

   Innocent Bashungwa ambae Waziri wa viwanda wakati wa ziara yake ya kukagua viwanda vilivyopo wilayani Tabora, lakini katika kiwanda cha uzalishaji nyuzi cha TABOTEX ameonyesha kutorizishwa na uzalishaji wa kiwanda hicho pamoja na utendaji wake.
       Aidha,Waziri Bwashungwa akiwa katika kiwanda hicho cha nyuzi huku akiangalia uzalishaji katika kiwanda hicho ambacho kilibinafsishwa kwa muwekezaji wa familia ya Raja  mnamo mwaka 2004 kikimilikiwa na Serikali lakini kikiwa na uwezo wa kuajiri wafanyakazi zaidi ya mia mbili ambapo uzalishaji wa nyuzi kwa mwaka ulikuwa takribani ya tani elf tatu na mia sita,ambapo kwa sasa uendeshaji wa kiwanda hicho ni kinyume na Serikali ilivotarajia.












  Mbunge wa jimbo la Tabora mjini Emanueli Mwakasaka ameeleza kuwa kiwanda hicho kingekuwa na hatua nzuri iwapo kingeenda na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.
  Lakini,hata hivyo Waziri Bashungwa  ametembelea katika kiwanda cha misitu Tabora pamoja na kiwanda cha maziwa ambapo ametoa agizo wakati akiwa kwenye  kiwanda hicho cha maziwa ameiagiza shirika la kuhudumia viwanda vidogo SIDO kuwaunganisha wawekezaji wadogo na kampuni kubwa ili waweze kuimarika zaidi pia amekitaka kiwanda cha nyuzi-TABOTEX kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano.
     Na Mwandishi wetu;Adolf Mwingira.
 

No comments

Powered by Blogger.