Header Ads

Header ADS

Watu Wawili Wamejeruhiwa Kaika Jaribio la moto mkoani katavi.

   Watu wawili wamejeruhiwa katika jaribio la moto lililoandaliwa na meneja wa huduma kwa wateja tawi la NMB mkoa wa katavi wakijaribu kujiokoa.
   Akizungumza na vyombo vya habari katika tukio hilo Hygrace Mwanjuguja ambaye ni Meneja amesema lengo la kuanda  jaribio hilo nikutaka kuona uharaka wa Jeshi la zimamoto pindi tatizo linapotokea.
 
   Mwanjuguja amesema  kuwa, hawakua na lengo baya la kuandaa jaribio hilo licha ya kusababisha majeruhi  ambao hadi sasa hali zao zinaendelea  vizuri na waliojeruhiwa mmoja ni muhudumu wa pale Pamoja na mteja na tayari wamepelekwa Hospitali  kwa matibabu zaidi.
   Pia,  Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Katavi, Islael Kutika amedai kuwa baada ya kupigiwa simu walifika eneo la tukio ndani ya dakika tano na kudhibiti moto ambao haujaleta madhara makubwa.
   Kutika amesema mpaka sasa hakuna uharifu wowote ambao umetokana na moto huo  tofauti na majeruhi wawili.

No comments

Powered by Blogger.