Header Ads

Header ADS

Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) kimewatunuku maofisa wa polisi 13 kutoka Ghana, Kenya na Zambia, kwa juhudi zao za kutuliza hali ya nchi.


Kamishna wa kikosi hicho Augustine Magnus Kailie aliyewatunuku maofisa hao nishani na vyeti, amewasifu maofisa hao kwa kuunga mkono juhudi za kuliunda tena jeshi la polisi la Somalia ambalo litahakikisha sheria na utaratibu wakati kikosi cha AMISOM kitapoondoka kutoka nchini Somalia.

No comments

Powered by Blogger.