Header Ads

Header ADS

Solskjaer anatumai bado ataendelea kuifunza Man United kwa mechi itakayofuata baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa dhidi ya Watford. (Guardian)

 Rio Ferdinand, mshindi mara sita wa Ligi ya Premia akiwa na Manchester United, ametoa wito kwa klabu yake ya zamani kumfuta Solskjaer kufuatia matokeo mabaya ya klabu huyo. (YouTube, via Mirror)
Watford na Newcastle wanapania kumsajili kwa mkopo mlizi wa Manchester United na England Phil Jones, huku klabu kadhaa kubwa zikimuwania kiungo hiyo wa miaka 29. (Sun)
Dean Smith,aliyetimuliwa na kama kocha wa Aston Villa wikendi iliyopita huenda akarejea uwanjani hivi karibuni baada ya klabu ya Norwich City kuonesha nia ya kutaka kumsajili kama meneja wao mpya. (Telegraph, subscription required)
Kocha wa zamani wa Chelsea Frank Lampard pia anapigiwa upato wa kuajiriwa na Norwich, pamoja na Ralph Hasenhuttl wa Southampton . (Sky Sports)
Kiungo wa kati wa Uhispania Saul Niguez, 26, anajiandaa kusalia Chelsea kwa mkopo wa msimu mzima kutoka Atletico Madrid, licha ya kucheza kwa dakika mbili tu katika Ligi ya Primia tangu alipojiunga nao mwezi Agosti (Telegraph, subscription required)
Tottenham watalazimika kulipa Fiorentina £60m kuwapiku mahasimu wao wa London kaskazini Arsenal katika usajili wa mshambuliaji wa Serbia Dusan Vlahovic, 21. (La Nazione, via Express)
Kiungi wa kati wa Arsenal na England Ainsley Maitland-Niles, 24, anasema sasa yuko radhi kusalia katika klabu hiyo baada ya kujaribu kuondoka wakati dirisha la uhamisho lilipofunguliwa msimu wa joto. (PA Media, via Mail)

Newcastle United wanataka kumsaini kipa wa Lazio na Albania Thomas Strakosha, 26, dirisha la uhamisho wa msimu wa baribi litakapofunguliwa. (Sun)

No comments

Powered by Blogger.