Header Ads

Header ADS

Urusi imeweka idadi kubwa ya Majeshi na Vifaa mpakani na Ukraine

 Wakati dunia ikiendelea kushuhudia mzozo wa wahamiaji katika mpaka wa Belarus na Poland, hali nyingine ambayo inaweza kuleta mtafaruki inatokea mashariki mwa Ulaya.

Kwa siku kadha, Urusi imeanza kuongeza idadi ya wanajeshi na silaha zinazoenda katika mpaka wa Ukraine, kufikia mpaka serikali nyingine ikiwemo Marekani na Umoja wa Ulaya kutoa angalizo la shambulio wakati wa baridi.

Kiev na Moscow wamekuwa katika vita kwa kipindi cha zaidi ya miaka saba wakati Putin alipoivamia na kuiteka Crimea na mgogoro wa mpakani huku wanajeshi wa Urusi wakiwa katika eneo hilo kila mara.

Uhalisia ni kuwa msimu uliopita ,angalizo lilitolewa wakati Urusi ilipopeleka silaha katika mpaka wa Ukraine.

Hata hivyo , vyanzo kadhaa vya kijasusi vya nchi za magharibi vimeeleza wasiwasi wao kuhusu hali ilivyo kwa sasa.

Wizara ya Ulinzi ya Ukraine inakadiria kuwa zaidi ya wanajeshi 114,000 wa Urusi wamepelekwa katika eneo la mpaka kaskazini-mashariki, mashariki na kusini mwa Ukraine, ikiwa ni pamoja na askari wa kawaida 92,000 , wanaanga na wanamaji.

Wiki iliyopita Washington ilidai kuwa na ripoti za kijasusi ambazo zilionesha kwamba Kremlin ilikuwa "inajiandaa kwa uvamizi" na siku ya Jumatatu mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg, alitoa wito wa kuzingatia "mkusanyiko mkubwa wa jeshi la Urusi.

Tunaona mkusanyiko usio wa kawaida wa askari na tunajua kwamba Urusi imekuwa tayari kutumia aina hii ya uwezo wa kijeshi kabla ya kufanya vitendo vya kichokozi dhidi ya Ukraine," Stoltenberg alisema katika mkutano wa waandishi wa habari.

Siku ya Jumanne, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alizungumza na mwenzake wa Urusi kueleza namna ambavyo Ufaransa iko tayari "kutetea mamlaka ya eneo la Ukraine," wakati Ujerumani pia ikionya "matokeo makubwa" katika tukio ambalo Moscow ilishambulia nchi hiyo jirani.

Awali, mkuu wa Majeshi ya Uingereza, Jenerali Nick Carter, aliliambia gazeti la Times kwamba Uingereza inapaswa "kuwa tayari" kwa vita na Urusi.

Ikulu ya Kremlin haijakanusha hatua hizo za kijeshi, lakini imesema mapendekezo ya uchochezi na imeilaumu NATO kwa kufanya mazoezi ya kijeshi katika pwani ya Crimea.



No comments

Powered by Blogger.