Header Ads

Header ADS

mwenyekiti wa wakurugenzi simba sc amesema hana hofu na kikosi chao

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba SC Salim Abdallah ‘Try Again’ amesema hawana shaka na kikosi chao katika michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu huu 2021/22.

Simba SC inaongoza msimamo wa ‘Kundi D’ kwa kufikisha alama 07, baada ya kuibanjua RS Berkane bao 1-0 Jumapili (Machi 13), Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Try Again amesema Uongozi wa Simba SC umekua ukifanya kazi zake kwa umakini mkubwa ili kutimiza lengo la kikosi chao kupata ushindi, na hilo limekua likitokea, hivyo wachezaji wanajua majukumu yao.

Amesema kwa mfumo huo, anaamini Simba SC itafika mbali kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika, huku akikumbushia mipago yao ni kufika Nusu Fainali na ikiwezekana kutinga Fainali na Kutwaa Ubingwa.





No comments

Powered by Blogger.