Bi.Kevela: Wanawake UWT acheni kupanga safu ya uongozi
Wanawake wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania mkoani
Njombe, wameagizwa kuacha kupanga safu ya uongozi badala yake watende haki
katika chaguzi za ndani zinazoendelea nchini na katika mkoa huo.
Agizo hilo lometolewa na Mwenyekiti wa jumuiya ya umoja
wa wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Njombe Scolastika Kevela, alipokutana na
viongozi wa jumuiya hiyo katika ziara yake aliyoifanya katika wilaya ya Ludewa
ili kutoa maelekezo mbali mbali juu ya Chama na Jumuiya.
“Katika chaguzi tunazoendelea nazo,tuache kupanga safu
kwasababu ukiona mtu anafanya hivyo maana yake mtu huyo hajiamini na kwa muda
wote hajafanya kazi akisubiri nyakati za uchaguzi,kiongozi wa namna hiyo ni
kumpiga chini”amesema Scolastika Kevela
Aidha Bi,Kevela ametoa wito kwa wananchi na wanawake wa
mkoa huo kuendelea kulea familia kwa bidii ili kuondokana na tatizo la utapiamlo
kwa kuwa mkoa huo upo imara kiuchumi.
“Tukalee familia zetu kwa bidii ili tuondokane na mdudu
anayeitwa utapiamlo na kama sio wewe basi ukimwona jilani yako mwambie”alisema
Bi,Kevela
Baadhi ya wanawake akiwemo Ester Mwalongo na Reinihada
Tweve wamekiri kuwa nyuma katika maswala ya malezi kwa watoto na kusababisha
utapiamlo kutokana na kuwa bize katika kazi huku wakiwa na uchumi mzuri.
Related Posts
-
Next
Simon Msuva: Tuna kumbukumbu nzuri hapa Benin
-
Previous
Rais Biden amelihutubia taifa akiliomba bunge kuidhinisha sheria kudhibiti vifo vya bunduki
No comments
Post a Comment