Header Ads

Header ADS

CHADEMA: Katibu mpya Kanda ya Kati ataja vipaumbele vitatu

katibupic

Katibu mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kati, Emmanuel Masonga ametaja vipaumbele vitatu atakavyoanza navyo katika nafasi yake hiyo mpya.

Hivi karibu Kamati Kuu ya Chadema ilifanya uteuzi wa Makatibu wapya wa Kanda ambapo Masonga aliyekuwa Kanda ya Nyasa aliteuliwa  kwenda Kanda ya Kati  huku aliyekuwa Kanda ya Kati, Gwamaka Mbugi akipelekwa Kanda ya Nyasa.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya ofisi na Katibu aliyepita,  Masonga  amewaomba wanachama wa CHADEMA wa ya kanda hiyo wawe na umoja na wapendane.

 “Naomba tupendane mapokezi haya ni uthibitisho kwamba hapa kuna upendo,mimi ni muumini wa ushirikiano ili tufanye mambo makubwa kwa ajili ya chama chetu,nataka maendeleo,nataka chadema izidi kusonga mbele”

Kwa upande wake, Mbugi amewaomba wanachama wa chama hicho kumpa ushirikiano Gwamaka kama walivyokuwa wakimpa yeye.

“Kuna yale ambayo tulipishana naomba radhi naondoka Kanda ya kati nikiwashukuru kwa jinsi ambavyo mmenipa ushirikiano mkubwa nasema asanteni sana,”amesema.

Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Singida, Jingu Emmanuel amewaomba Makatibu hao kutenda haki katika utendaji wao wa kazi  bila ya kumwonea mtu huku akiahidi kumpa ushirikiano Katibu mpya wa Kanda hiyo Masonga.

Mwenyekiti wa Chadema mkoani Morogoro, Jackson Malisa amesema anaamini mabadiliko hayo yataleta chachu ya maendeleo kwani Makatibu hao bado ni vijana na wana kesho nyingi.

 


No comments

Powered by Blogger.