Header Ads

Header ADS

CHADEMA yaitaka serikali kushusha bajeti kutoka trilioni 41


Chama cha Demokrasia na maendeleo ,CHADEMA, mhe, John kimeitaka  serikali kushusha bajeti kutoka trilioni 41 ambayo wameiwasilisha badala yake itengeneze bajeti kwa kadri ya uzoefu na uhalisia wa ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Tamko hilo limetolewa na Katibu mkuu wa chama hicho, mhe, John Mnyika wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi ni kasi ambayo hairidhishi,

“Kasi yetu ya ukuaji wa uchumi wan chi ni kasi ambayo hairidhishi, kuna sekta muhimu zenye kugusa maisha ya wananchi zinadondoka badala ya kuongezeka, hali ambayo inahitaji hatua za ziada za serikali kuinusuru nchi na hali hii,” alisema Mnyika

“Hiki ambacho serikali imejivunia bungeni kwamba kuna ukuaji wa uchumi kwa sababu tu la ongezeko la 0.1%, kutoka 4.8% mwaka 2020 mpaka 4.9% haistahili pongezi kwa serikali. serikali ieleze hatua zaidi ambazo zitachukuliwa ili kuongeza kasi ya ukuaji uchumi.” Mnyika

Aidha alisema bajeti ya serikali ilitakiwa kuindiza mradi wa katiba mpya na kupewa kipaumbele kwani ni mradi ambao taifa lilishaanza miaka mingi hapo nyumamnamo mwaka 2014 na tayari nchi imeshatumia mabilioni ya pesa.

Pamoja na hayo Mnyika amesema ripoti ya CAG ya mwaka 2021 kama zilivyo kwenye ripoti za miaka ya nyuma zimeanisha ufisadi mkubwa ndani ya serikali na ndani ya mashirika ya Umma, lakini hawajaona hatua zozote bungeni wakati wizara mbalimbali zinajadiliwa.

Ameongeza kuwa wakati taifa linapitia katika kipindi kigumu kiuchumi na wananchi wanapitia mazingira magumu serikali inapaswa iwe ya utekelezaji.

“Katika mazingira ambayo taifa linapitia kwenye hali ngumu kiuchumi na wananchi wanapita katika mazingira ya kufunga mkanda, wakati umefika sasa serikali kutekeleza mapendekezo yetu ya muda mrefu wa kupunguza ukubwa wa serikali” alisema Mnyika

“Bajeti ya serikali lazima ikizi vipaumbele na matakwa ya wananchi kwa kuzingatia siyo tu mipango ya muda mrefu ya nchi bali bajeti ya serikali lazima izingatie uhalisia  wa matakwa na mahitaji ya wananchi ya wakati huo bajeti inapitishwa”

Hatahivyo Alisema bunge halitekelezi majukumu yake huku akigusia suala la tozo za kidi ya mafuta kemba haviguswa,

"Bunge halitekelezi majukumu yake ya kuishauri na kuisimamia Serikali, michango inayoendelea sasa haiangazii mapungufu na udhaifu wa bajeti." Mhe.

"Kwa takwimu za Serikali tozo na kodi za mafuta kwa Petroli ni shilingi 920.68, Dizeli ni shilingi 813, mafuta ya taa ni shilingi 577. Eneo hili la kodi halijaguswa."Mhe Mnyika

No comments

Powered by Blogger.