Viwanja vitano kuwekwa Nyasi Bandia
Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan
imedhamilia kuviboresha viwanja vya michezo nchini kwa kuviwekea
Nyasi Bandia.
Uthibitisho huo umetolewa leo Jumanne (Juni 14) na Waziri wa
Fedha na Mipango Mwigulu Nhemba, alipokua akisoma makadirio ya Mapato na
Matumizi (Bajeti ya 2022/23) ya Serikali, Bungeni mjini Dodoma.
Waziri Nchemba amesema kwa kuanzia, Serikali itaanza kuviwekea
Nyasi Bandia viwanja vitano, na kisha vingine vitafuata.
“Kwa kuanzia tutaweka Nyasi Bandia katika viwanja vya mikoa ya
Mwanza, Dodoma, Arusha, Tanga na Mbeya” amesema Waziri Mwigulu Nhemba.
Kuboreshwa kwa viwanja vya CCM Kirumba, Sheikh Ameri Abeid,
Mkwakwani, Sokoine na Jamhuri kutanogesha ushindani zaidi katika Mshike Mshike
wa Michezo ya Ligi Kuu na madaraja ya chini kwa msimu ujao wa 2022/23.

No comments
Post a Comment